330. Tunakwenda Mbinguni

1. Tunakwenda mbinguni!

   Duniani twasafiri 

   wenye taabu nyingi, 

   mpaka tufike mbinguni.

   Hapa tu wapitaji,

   kule sisi wenyeji.

 

2. Ninakwenda mbinguni!

   Roho yangu; angalia

   mambo yaliyo ya juu; 

   usishikwe na dunia.

   Roho iliyong’azwa,

   na Mungu yampendeza.

 

3. Ninakwenda mbinguni,

   ndivyo ninavyoambiwa.

   Hili lanionyesha

   raha na furaha zote, 

   nitakazozipata 

   nikifika mbinguni. 


4. Ninakwenda mbinguni 

   kufa kutanipeleka

   pale nitakapokaa, 

   shida zikiisha zote. 

   Namfuata Mwokozi  

   aliyetangulia. 


5. Ninakwenda mbinguni 

   nitashika neno hili. 

   Nitashinda kabisa

   majaribu hata taabu, 

   nikikumbuka hivi: 

   ninakwenda mbinguni! 

 

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu