328. Ndugu, Kundi Lake Mungu
1. Ndugu, kundi lake Mungu
atupendaye sana,
tumfuate Mponya wetu
tukipendana vema.
Yeye kichwa, tu viungo,
Yeye nuru yetu kuu;
Yeye Bwana, sisi ndugu.
Atupenda, twampenda.
2. Njooni watoto wa Mungu,
sasa turudi kwake,
tumwapie: Sisi sote
twataka kukushika.
Na upendo wa kindugu
utakapolegea,
tutamsihi Bwana wetu
azidishe upendo.
3. Enyi viungo vya Yesu,
pendaneni kwa bidii,
kazeni kujipa mioyo
ya kuwafia ndugu.
Kama alivyotupenda
Yesu akatufia.
Nasi tusipopendana
ahuzunika sana.
4. Yesu uwaunganishe
watu wakupendao,
Wapendane kwa mioyo,
kama unavyotaka.
Watumikiane vema
na kufurahishana;
wawe wote kundi moja
na Wewe Mchunga wao.
Comments
Post a Comment