327. Mwokozi Yesu Asema

1. Mwokozi Yesu asema:

   Nifuateni nyote!

   Acheni ulimwengu huu, 

   utafuteni kwanza

   ufalme wa mbinguni tu 

   na haki yake kwa bidii.


2. Ninaing’aza mioyo,

   iweze kwenda sawa, 

   atakayenifuata, 

   haendi kwenye giza. 

   Natangulia Wakristo

   washike njia ya kweli.


3. Unyenyekevu na pendo,

   zajaa moyoni mwangu,

   na kinywa changu kimejaa,

   maneno ya upole.

   Nami namngojea Mungu 

   kwa haja zote za roho.


4. Naonyesha yanayofaa; 

   yafuateni vema 

   Itakaseni mioyo 

   isiwe na uchafu. 

   Nalinda roho za watu, 

   wafike kwangu mbinguni.


5. Atakaye kuiponya 

   nafsi, huipoteza; 

   aipotezaye nafsi

   atafika kwa Mungu.

   Asiyeuvumilia

   msalaba hanistahili.


6. Sababu hii tumfuate

   Bwana kwa nguvu zote. 

   Tuvumilie mateso

   kwa ajili ya Yesu.

   Asiyeshindana vema 

   hapewi taji ya mbingu. 

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu