326. Mbona Wasumbukia
1. Mbona wasumbukia
mambo ya ulimwenguni,
yaliwayo upesi,
yafananayo na taka.
Umtafute Yesu tu,
ukitaka furaha.
2. Zoeza roho yako
kufikiri mambo mema,
yaliyo ya mbinguni
na rehema yake Mungu.
Umtafute Yesu tu …
3. Mara nyingi wataka
kupumzisha moyo wako.
Iko chemchemi ya neema,
utakapopata raha.
Umtafute Yesu tu …
4. Ukimbie hatari
za ufalme wenye giza:
umchague Mwokozi
afurahishaye moyo.
Umtafute Yesu tu …
5. Kweli ulimwengu huu
unapenda mambo mengi
yasiyokupendeza
Yesu uliyetuita.
Umtafute Yesu tu …
6. Umezaliwa tena
kwa maji na Roho wake.
Basi usifuate
mambo ya mtu wa kale.
Umtafute Yesu tu …
7. Ukumbuke kwa bidii
utukufu wake Mungu,
inua moyo wako,
kwa kuomba na kusihi.
Umtafute Yesu tu …
8. Ukifanya hivi tu
hutakosa mwisho mwema,
Yesu akupendaye
atakupa utukufu.
Umtafute Yesu tu …
Comments
Post a Comment