323. Bwana Utusaidie
1. Bwana utusaidie
tuwe wanafunzi wako wazuri.
Utung’aze macho yetu,
utupe sote mioyo myeupe.
Tufuate njia zako,
tuwe wenye nia moja.
Twakuomba:
Uzidishe Nguvu kwetu.
2. Wote waona furaha,
wampendao
Bwana Yesu kwa moyo.
Nasi tuwe watu wake,
tuwe kama
shamba zuri la Yesu.
Anapenda kuingia
na kukaa mioyoni mwetu.
Umpokee ukitaka kuokoka.
3. Sikia kuomba kwetu
Yesu upendaye kutubariki,
Uzidi kutubariki, tusishindwe,
shida zikitujia.
Uongoze watu wako,
tufuate njia zako.
Mpaka tutakapoingia mbinguni.
Comments
Post a Comment