322. Mjini Kwake Babangu

1.  Mjini kwake Babangu 

    ndipo pa raha

    tutafika juu kwake

    tukae naye. 

    Kuna raha, Kuna raha.

    /:Kwake Bwana kuna raha:/ 

    Lini tutafika kwake 

    tuungane na malaika 

    mjini kwake, mjini kwake.


2.  Pale kwake Babangu 

    ndipo pazuri. 

    Siku ile kuu mno

    ya kupaona.

    Kuna raha. Kuna raha. 

   /:Kwake Bwana kuna raha:/ 

    Mji ung’arao mno

    ni makao ya malaika

    mjini kwake, mjini kwake.


3.  Nikipanda mlimani 

    na kuyaona 

    yote ya utukufu aliyofanya.

    Kuna raha. Kuna raha.

    /:Kwake Bwana kuna raha:/ 

    Yote yanisimulia 

    ufahari wake Baba

    mjini kwake, mjini kwake.


4.  Njoo mwenzangu tazama

    yote ya Mungu 

    yote ameyafanya kwa ajili yetu.

    Kuna raha. Kuna raha.

    /:Kwake Bwana kuna raha:/ 

    Tuinue macho yetu 

    tumtazame Mwumba wetu

    mjini kwake, mjini kwake.

Comments

Popular posts from this blog

276. Nina Haja Nawe

257. Haya ee Moyo Wangu

265. Mganga Wetu ni Karibu