320. Yesu Nakupenda, u Mali Yangu
1. Yesu nakupenda, u mali yangu,
anasa za dhambi sitaki kwangu
na Mwokozi aliyeniokoa,
sasa nakupenda, kuzidi pia.
2. Moyo umejaa mapenzi tele
kwa vile ulivyonipenda mbele
uhai wako ukanitolea
sasa nakupenda, kuzidi pia.
3. Ulipoangikwa msalabani
tusamehewe tulio dhambini;
Taji ya miiba uliyoivaa
sasa nakupenda, kuzidi pia.
4. Niwapo hai, niwapo maiti,
kupendana nawe kamwe siachi,
hari za kifo zikinienea,
sasa nakupenda, kuzidi pia.
5. Mawanda mazuri hata maskani
niyatazamapo huko mbinguni.
Tasema na taji nitakalovaa
sasa nakupenda, kuzidi pia.
Comments
Post a Comment